Monday, October 27, 2014
Usifanye Haya
Thursday, July 18, 2013
Anaumia Nikigusa
Thursday, October 11, 2012
Monday, September 19, 2011
Ujuzi katika Ndoa
Kama wewe ni kizazi cha Adam na Hawa basi suala la ndoa linakuhusu sana na ndoa ni kitu beautiful, Kwani huleta mahusiano ya kutosheleza yanayowaunganisha watu wawili mke na mume.
Inapendeza kwamba Mungu amemuumba mtu maalumu kwa ajili yako.
10. UJUZI WA KUTATUA MATATIZO
Kama wanandoa hawana ujuzi wa kutatua matatizo inaweza kusababisha ndoa kuwa ngumu sana hasa miaka 2 ya kwanza katika ndoa.
Kuwa na ujuzi namna ya kutatua matatizo katika ndoa ni kufahamu namna ya kuzozana kwa kuelezana ukweli kwa upendo, kufahamu ni wakati gani wa kukaa kimya au kuzungumza.
9. UJUZI WA KUMWEKA MWENZI WAKO NAMBA MOJA
Kumbuka katika ndoa kuna wewe, mwenzi wako na Mungu.
Jambo la msingi ni uhusiano wako na Mungu wako (siyo kazi ya Mungu, au kwenda kanisani bali uhusiano wako na Mungu, then mwenzi wako (mume au mke) ndipo wanakuja watoto na mwisho kazi.
Kama mke wako anafuata baada ya watoto, mama yako au baba yako au ndugu zako au rafiki zako au TV au Manchester United au chochote kile basi ndoa yako haina jipya na ipo siku mwenzi wako ataona hana maana katika ndoa yenu.
8. UJUZI WA KIMAISHA
Ni muhimu sana kila mwanandoa kufanya vitu ambacho vitakuwa msingi wa maisha ya baadae (future) pia kila mwanandoa analo jukumu la kujiuliza ni namna gani anaweza kuwa mwanandoa mwema miaka 10 au 20 ijayo.
Kila mwanandoa analojukumu la kujiuliza nifanye vitu gani ili niwe mwenye mvuto hata miaka 10 ijayo.
Je, niende shule?
Je, nianzishe biashara?
Je, nifanyeje kumpa support mwenzi wangu katika kazi zake au taaluma yake?
7. UJUZI WA KUSAMEHEANA
Unapokuwa kwenye uchumba, mchumba akifanya kitu cha ajabu unaweza ukaachana naye na kumsahau kabisa, hata hivyo kwenye ndoa unatakiwa kusamehe na kusahau sasa hivi.
Mwenzi wako anapofanya kitu na kujiona amekosea, atakuomba msamaha Kwani ni kweli yeye ni binadamu na ana mapungufu na hayupo sahihi mara zote.
Muda ule ambao unakuwa hutaki kusamehe mahusiano huacha kukua na hudumaa.
Kama huna uwezo/moyo wa kusamehe basi kwenye ndoa usiingie; jibakie single milele.
6. UJUZI WA KUWA MBUNIFU
Kwenye ndoa tunaishi pamoja na kuonana kila siku, tunalala pamoja, kula pamoja, oga pamoja nk.
Bila kuwa mbunifu kuwa na “fun stuff” ndoa huzoeleka na kuchosha.
Tafuta vitu ambavyo mkifanya pamoja vitawafanya kuwa na kitu kipya.
Wapo wanandoa ambao akioa au kuolewa basi Hakuna jipya, Hakuna ubunifu kila mwaka vitu ni vilevile, badilika fanya vitu Tofauti kama hujawahi kwenda sehemu fulani nenda na mkeo au mumeo, have fun!
5. UJUZI WA MTAZAMO CHANYA
Jifunze kuwa na mitazamo chanya kwenye tabia za mwenzi wako. Ni kweli kuna vitu unavipenda kuhusu yeye na kuna vitu ambavyo unavichukia kuhusu yeye, hata hivyo ukweli ni kwamba vitu vizuri unavyovipenda kuhusu yeye ndivyo vimekufanya uoane naye na kwamba vina nguvu kuliko vile ambavyo huvipendi kuhusu yeye.
Weka mtazamo (focus) kwenye vile vitu ambavyo vinawafanya ninyi wawili kuwa kitu kimoja.
Ukimnyoshea kidole kimoja mwenzi wako, basi unatakiwa kujinyoshea vidole 5 wewe mwenyewe.
4. UJUZI WA KUJIAMINI
Lazima uamini kwamba ndoa yenu itadumu na Hakuna kitu kinaitwa talaka na talaka haitakubalika.
Ni muhimu sana ujiamini kwamba mwenzi wako ( mume wako au mke wako) anakipenda sana kama wewe unavyompenda yeye hata kama haoneshi kwamba anakipenda.
Fahamu hivyo na amini hivyo.
Kwa njia hii huwezi kuyumbishwa na upepo wa mashaka na hofu wakati kunajitokeza kutoelewana.
Kwa njia hii itakuwa rahisi kuirudisha ndoa kwenye mstari.
3. UJUZI WA KUJIFUNZA
Wakati mwingine katika ndoa huwa tunajidanganya sana kwamba tunawafahamu vizuri wenzi wetu hata hivyo baada ya muda tunaanza kushangaa na kujiona tumeoana na mtu ambaye amebadilika sana na Tofauti na wakati ule mnaoana.
Hata hivyo kujisikia mume wako au mke wako amebadilia na kuwa binadamua mwingine si Sababu ya kuachana au kupeana talaka.
Kama huna ujuzi wa kumsoma au kujifunza kuhusu mwenzi wako basi hukutakiwa kuoa au kuolewa au hukustahili kuoa au kuolewa naye.
2. UJUZI WA KUJUA NAMNA WENGINE WANAWAONA/WANAJIFUNZA
Kama umeoa au kuolewa na unajifanya hujaoa au kuolewa ni kweli dunia na viumbe wake wanakuona ni kweli hujaoa au kuolewa pamoja na umri wako kwenda.
Unatakiwa kuonekana wewe na mwenzi wako ni watu wenye furaha na amani na kweli iwe furaha na amani ya kweli siyo fake.
Mnatakiwa kuwa na smile la kweli na liwe na kweli si fake.
Lazima uwe makini na kufahamu wengine wanawaonaje kama wanandoa na hiyo itakusaidia kujiweka sawa kuhakikisha kunakuwa na kicheko katika ndoa yenu.
1. UJUZI WA NAMNA YA KUGOMBANA
Hakuna ndoa ambayo wanandoa hawajawahi kupishana au kupingana au kutoelewana au kutokukubaliana katika jambo fulani au tabia fulani.
Pia ni muhimu sana kufahamu kila mnagombana au Sababu ya kitu kinafanya kuwe na msuguano.
Unatakiwa kuwa na ujuzi wa kufahamu kwamba kugombana kokote kusiwe kwa masaa kadhaa, au siku kadhaa au miezi kadhaa.
Pia ni muhimu sana kuangalia namna unabishana au unaongea wakati wa kutokukubaliana na jambo lolote.
Pia focus katika kulishambulia Tatizo lenyewe na siyo mwenzi wako.
Thursday, August 25, 2011
Kileleni!
Katika ndoa sex ni kitu kizuri kinachowafanya wanandoa kuwa mwili mmoja kwa maana ya kuwaleta karibu.
Jambo kubwa ambalo huleta raha ya kiwango cha juu kwa wanandoa wakati wa tendo la ndoa ni suala la kufika kileleni (orgasm)
Kila mwanandoa anaweza kufika kileleni Ingawa si kila mmoja, kufika kileleni kwa wengine si issue rahisi hasa kwa wanawake Ingawa kwa wanaume ni kitu rahisi hata kitendo cha mwanaume kuwa na penetration na kuingia kwa mke wake basi anaweza kujikuta anafika kileleni, Ingawa hilo haliwezi kumfanya mwanamke kufika kileleni.
Kufika kileleni ni nini?
Ni kitendo cha kufikishwa juu kabisa katika raha ya sex, msukumo wa kiwango cha juu wa raha ya tendo la ndoa ambalo huishia kumwacha muhusika ajisikie yupo relaxed na mwepesi. Kwa mwanamke kufika kileleni huwa kwa sekunde kadhaa ambazo huendana na kujisikia relaxed na msukumo wa kutamani kama kunyanyuka ili kupokea kitu au kutoa hata hivyo kama mwanamke ataendelea kusisimuliwa huweza kujikuta anafika kileleni tena Ingawa hii ni kwa wanawake wa umri fulani.
Je kuna aina ngapi za kufika kileleni kwa mwanamke?
Kimsingi kuna aina mbili za mwanamke kufika kileleni na hizi aina zinajikita kutokana na aina ya msisimko anaoupata (stimulation).
Kwanza ni kifika kileleni kwa njia ya kusisimuliwa kisimi chake (clitoral) kwa mwanaume kukisisimua kwa kuchezea kwa njia Tofauti anazozijua au wanazoelekezana wakati wa tendo la ndoa.
Pili ni kufika kileleni kwa njia ya uke (vaginal) na hii mara nyingi hutokea kutokana na mwanaume kuingia na kutoka kwa mawimbi huku akigusa eneo la G-Spot
Uzuri ni kila aina ya kufika kileleni ina ladha yake na wanawake wenye uzoefu wa hizi aina wanafahamu Tofauti yake.
Ni wanawake wachache sana hufika kileleni kwa kitendo cha Mr. Happy kuwa ndani ya uke hata hivyo ni rahisi mwanamke kufika kileleni kwa kuchezewa kisimi/kinembe chake kwa namna zote (touching/rubbing or kissing)
Je, ni milalo ipi husaidia mwanamke kufika haraka kileleni?
Kwanza ni ule wa mwanamke kuwa juu ya mwanaume na pile ule wa mwanamke kulala kwa tumbo lake na mwanaume kumuingia kwa nyuma.
Je ni mambo gani yanaweza kuathiri mwanamke kufika kileleni?
KWANZA
Mara ngapi mwanamke anapata sex, ili mwanamke kufika kileleni anahitaji kuwa na sex ya mara kwa mara (use it or loss it). Mwanamke anapokaa kwa muda mrefu bila sex ndivyo anakuwa mgumu kusisimka na mgumu kufika kileleni period.
PILI
Lazima mwanamke awe relaxed na hana stress au tension. Ili mwanamke apate raha ya mapenzi ni lazima awe comfortable na mazingira yaliyopo na pia mahusiano au ndoa yake bila trust na mwenzi wake mwili unajifunga na ngumu kufungua.
TATU:
Hii inamuhusu mwanaume ambaye anahusika na huyu mwanamke anayetakiwa afike kileleni Kwani anatakiwa kuwa caring na anayefahamu kumsisimua mwanamke asisimke kiasi cha kutosha na kumsaidia kufika kileleni kwa kusoma upepo unavyovuma.
Pia ni vizuri kwa mwanamke mwenyewe kujitambua na kufahamu mwili wake vizuri na zaidi kushirikiana na mume wake kuwa wazi kumweleza kile anaona kinampa raha na kitapelekea kufika kileleni.
Je, unahitaji sex inayosisimua katika ndoa soma hapa
Tuesday, August 23, 2011
Nimpe?
Je, ni muhimu wanandoa kusalimiana mnapoamka asubuhi?
Kwanza fahamu kwamba wanandoa wanapokaa muda mrefu baadhi ya vitu huanza kuchakaa kimapenzi. Hata hivyo upendo na wema husaidia kurudisha moto wa mapenzi na wanandoa kujiona wapya kila umri unavyozidi kuongezeka.
Matendo yanayoonesha wema kwa wanandoa ni gundi inayoshikisha wawili kujiona wapo karibu na moja ya tendo la wema ni kumsalimia mwenzako wakati mnaamka hata kama mmelala kitandani kimoja na hata mlikumbatiana usiku mzima au ulimuweka mwenzi wako kifuani usiku mzima.
Anayesalimiwa hujiona anapendwa, ana thamani na pia appreciated.
++++++++++++++++++++++++++
Tupo kwenye new millennium kiasi ambacho watu tupo busy hata kuamka tunahitaji kuweka alarm ituamshe hata hivyo badala ya kukimbia bathroom kuoga ni muhimu kumpa kwanza salamu mwenzi wako ndipo uendelee na kazi zingine au na ratiba yako.
Tafiti zinaonesha wanandoa ambao husalimiana asubuhi wanajiona ndoa yao ni nzuri sana na wana mahusiano yanayoridhisha.
++++++++++++++++++++++++++++++++
Je, nini kinafanya maneno ya salaamu ya asubuhi kuwa muujiza katika ndoa na mahusiano?
Unapomsalimia mwenzi wako maana yake unamwambia na kumpa ujumbe kwamba ni asubuhi njema tumeamka pamoja katika upendo na furaha na kwamba unajisikia vizuri kuanza siku mpya na mtu wako na pia unaweza msingi mzuri wa mawasiliana kwa hiyo siku mpya.